Tuesday, 13 September 2016

UEFA YATIMUA VUMBI HATUA YA MAKUNDI



LIGI YA KLABU BINGWA BARANI ULAYA jana ilianza ambapo jumla ya michezo saba kwenye makundi matano  ilipigwa kwenye viwanja tofauti.

Amabapo kundi A Basel ya nchini uswiz ilitoshana nguvu kwa kutoka suluhu ya moja kwa moja na Ludogorets Razgrad ya nchini bulgaria, PSG ikiwa nyumbani ililazimiswa sare ya bao 1-1 dhidi ya washika bunduki wa london Arsenal, huku PSG wakitangulia kupata goli la mapema mnamo dk ya 1 ya mchezo kupitia mshambuliaji wake Edinson Cavani huku Goli la kusawazisha kwa upande wa arsenal likivungwa na Alexis Sanchez kwenye dk ya 78.

Tukio kubwa katika mchezo huo ni kadi mbili nyekundu zilizotolewa kwa timu zote mbili, Olivier Geroud akipewa kadi nyekundu kwenye dk ya 90 ya mchezo baada ya kadi ya njano aliyopewa kwenye dk ya 88, huku kwa upande wa PSG Marco Verratti nae pia akiambulia kadi nyekudu kwenye dk hiyo hiyo ya 90 baada ya kadi ya njano aliyopewa kwenye dk ya 8.

Lakini matokeo makubwa waliyapata Barcelona baada ya kubamiza Celtic kwa idadi ya magoli 7-0 huku messi akianza na hat- trick, magoli mengine yalifungwa na Suarez ambaye alipachika magoli mawili, Neymar na Iniesta wakipata goli moja moja. Huku Mousa Dembele akikosa mkwaju wa Penalt kwa upande wa Celtic 

Na mchezo mwengine wa kundi D Bayern Munich ilicharanga FC Rostov ya nchini Urusi Magoli 5-0 huku Atletico Madrid ya nchini Uispania ikiwa ugenini iliibuka na ushindi mwembamba wa goli 1-0 dhidi ya mwenyeji wake PSV Eindhoven ya nchini uholanzi


Mechi nyengine ni  
Benfica1 - 1 Besiktas
Dynamo Kyiv1 - 2 SSC Napoli

Image result for MESSI



No comments:

Post a Comment