Wednesday, 14 September 2016

MICHEZO MCHANGANYIKO




Meneja wa mashetani wekundu Jose Mourinho amesema michuano ya Europa inaweza kuathiri timu yake malengo ya ubingwa wa ligi kuu ya England . lakini bado anataka kushinda kwenye hatua ya pili ya michuano hiyo ya Europa na atahakikisha wachezaji wake wanakuwa tayari kwa pambano.

Kikosi cha Man.U kikiwa na wachezaji 20 bila nahodha wao wayne rooney kikiwa ugenini leo hii kitakipiga na fayenoord ya uholanzi
Ligi ya klabu bingwa barani ulaya imeedelea kutimua vumbi usiku wa kuamkia leo ambapo kulikuwa na michezo tisa ikipigwa katika viwanja tofauti.

KATIKA USIKU WA KLABU BINGWA KUAMKIA LEO

Matajiri wa london Manchester City wakiwa nyumbani waliibuka na ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya Borussia Moenchengladbach, hatrick ya Kun Aguero na goli moja la Kelechi Iheanacho yalitosha kuipatia man.city point tatu na kuwa timu ya pili kwenye msimamo wa kundi C ambalo linaongozwa na Barcelona

Tottenham Hotspurs ikiwa nyumbani ilikubali kipigo cha magoli mawili kwa moja dhidi ya Monaco ya nchini Ufaransa ambayo inaongoza ligi kuu nchini humo
Lakini usiku wa kuamkia leo ilikuwa ni kicheko kwa wachezaji na washabiki wa Leicester City
 Kwani wakiwa ugenini waliipiga Club Brugge ya ubelgiji jumla ya magoli 3-0 huku Riyad Mahrez akitupia mawili.

Borussia Dortmund ikiwa ugenini iliidhalilisha Legia Warszawa ya Poland kwa dozi ya magoli 6-0

Na katika mchezo uliowastaajabisha wengi ulikuwa ni mchezo kati ya Real Madri dhidi ya Sporting CP Lisbon ya ureno ambapo Madrid iliibuka na ushindi wa magoli 2-1.

Sporting Lisbon ilikuwa ya kwanza kuandika goli la kwanza kwenye dk ya 48 goli lililodumu hadi dk ya 89 ya mchezo ambapo C.Ronaldo aliisawazishia timu yake kwa freekick maridi kabisa iloenda moja kwa moja kimyani, sekunde chache kabla mpira kumalizika Alvaro Morata aliiandikia Real Madrid goli la pili akiunganisha krosi ya James Rodriguez.





No comments:

Post a Comment