Pages

Sunday, 25 September 2016

HABARI MCHANGANYIKO




Balozi wa marekani katika umoja wa mataifa, Samantha Power ameituhumu urusi kwa kuzungumza uongo uliodhahiri kuhusu hatua yake nchini syria. Amesema kuwa warusi hawakushirikishwa katika kupamana na ugaidi nchi Syria. Bi Power aliliambia baraza la usalama la umoja wa mataifa kwamaba urusi na Syria wanatekeleza vitendo vyote vya kimabavu dhidi ya upinzani uliopo mashariki mwa Alepo, ndipo hapo uhalifu wa kivita unaweza kutekelezwa kwa kirahisi. Kwa upande mwengine Balozi wa Urusi, Vitaly Churkin, amewatuhumu waasi kwa kuvunja makubaliano ya kusitisha vita amabyo yalishindikana ndani ya muda mchache tu. Na muwakilishi wa Syria ameliambia baraza hilo la usalama kwamba jimbo lote la Alepo litarudishwa mikononi mwa serikali.

Umiliki wa jimbo la Alepo kwa waasi umeendelea kupungua ikiwa ni jitihada za urusi kuinga mkono serikali ya Syria katika kutekeleza mashambulizi dhidi ya waasi. Watoa huduma za matibabu wamesema kuwa wameshuhudia mashambuliza ya anga katika maeneo jirani ya kusini mwa mji huo. Mdadisi wa haki za binadam wa Uingereza aliyepo nchinim Syria amesema kuwa zaidi ya watu 20 wameuwawa, na kiasi hicho cha mauwaji kinatarajiwa kuongezeka. Kuna baadhi ya wakazi wamezingirwa na kifusi katika majengo yaliyoharibiwa, na watowa huduma za matibabu kwa mara nyengine wamezidiwa.

Wapiga kura wa uswizi wameidhinisha sheria ya kuipa nguvu ya ziada kitengo cha ujasusi cha nchi hiyo. Matokeo ya mwisho ya kura yameonesha kuwa takriban asilimia 66 ya kura wameunga mkono. Sheria hiyo itaruhusu mamlaka kuchunguza simu,kufuatilia shuguli za mitandao na kutumia kamera za siri na vipaza sauti kumchunguza mshtakiwa. Mwandisi wa BBC anasema kwamaba katika kipindi kilichopita Uswizi ilikuwa na wasiwasi kuhusu kuongeza mamlaka ya ufatiliaji ya nchi. Lakini shambulio la kigaidi la hivi karibuni lililotokea nchi jirani ya Ufaransa limebadilisha fikra za watu wengi.

Wabosnia na Waserbia wamepiga kura ya kuamua kwamba Januari tisa iwe ni siku ya mapumziko au la licha ya kuwa kura hiyo imepigwa marufuku na mahaka ya juu nchini Bosnia. Tarehe hiyo inahusiana na siku ya karamu kwa  wakiristo wa madhehebu ya Othodox,  na mahakama imesema kuwa huo ni ukandamizaji dhidi ya waisilamu wa Bosnia na wakiristo wa mahdhehebu ya katoliki wa Krosia wanaoishi nchini Serbia. Januari tisa pia ilikuwa ni tarehe mwaka 1992 amabayo Serbia iliwatangazia uhuru wa Croshia ndani ya Bosnia, iliyopelekea mtafaruku wa kimaadili. Mwandishi wa BBC  nchini Serbia anasema kuwa sheria hiyo imeandaliwa ili kuchochea uchaguzi wiki ijayo.

Rais Francois Hollande amekiri kuwa ufaransa iliwatelekeza walgeria walipigana vita wakiwa upande wa Ufaransa wakati wa Vita ya uhuru ya Ageria iliyodumu miaka nane iliyomalizika mwaka 1962. Makumi kati ya maelfu ya wa Algeria waliojitolea kwenye vita wajulikanao kama ‘hakins ’ waliwawa kama wasaliti baada  ya Ufaransa kuondoka Algeria. Wale wote waliofanya hivyo kwa ajili ya Ufaransa walihifadhiwa kwenye kamabi. Katika sherehe mjini Paris ikiashiria siku ya kitaifa ya kuwaheshimu waliojitolea kwa vita, rais Hollande alisema ufaransa inabeba lawama kwa jinsi walivyofanyiwa. Vizazi vyao walitafuta kwa muda mrefu utambuzi rasmi wa dhuluma.  

waziri wa mambo ya nje wa somalia, Abdisalam Hadliyeh anasema kwamamba  kundi la wapiganaji wa kiislamu la Al Shabaab limeshindwa kijeshi, kwa ushirikiano wa jeshi la Somalia na vikosi vya kulinda Amani vya umoja wa Afrika. Waziri  huyo amesema kwamba Al Shabaab kwa sasa wanamiliki chini ya asilimia kumi ya nchi nzima , na viongozi wake wengi wameuwawa au kukimbia katika miezi ya hivi karibuni. Hadliyeh amesema kuwa jambo lililopelekea utulivu wa muda mrefu ni kuwa na vifaa vizuri, mafunzo ya kijeshi na kufadhiliwa vikosi vya usalama vya taifa. Mchambuzi wa BBC wa masuala ya Afrika anasema kwamba licha ya kuwa kundi hilo limetokomezwa kwenye mji mkuu wa  Mogadishu, lakini bado linaendesha mashambulizi ya mara kwa mara mjini hapa na kwengineko. 

Polisi nchini hungary wanasema mlipuko wa Budapest usiku wa jumamosi uliowajeruhi maafsa wawili wa polisi ulisababishwa na bomu la kienyeji. Mkuu wa jeshi la polisi wa hungary   Karoly Papp amesema afsa wa palisi aliyekuwa kwenye patro akitembea kwa miguu alilengwa na shambulio hilo. Kwasasa wapo katika hali nzuri wakiwa Hospitali. Mtu anaeshtumiwa kutekeleza shambulio hilo, anaelezewa kuwa  ni kijana wa miaka ishirini bado hajapatikana.

Tamasha nchini Urusi la mpiga picha anyetatanisha wa marekani  limefungwa baada kupingwa na wanaharakati. Picha ziliyopigwa na Jock Sturges inajumuisha picha zinazomwonyesha mtoto akiwa mtupu. Seneta wa kihafidhina mwenye ushawishi mkubwa na mshauri wa serikali kwa masuala ya watoto wote wamelielezea tamasha hilo kuwa ni tamsha la ngono ya watoto na wametaka kufungwa kwa tamasha hilo. Mashuhuda wanasema takriban wnaharakati ishirini  waliojiita kuwa ni maafsa wa Urusi walilifunga tamasha hilo mjini Moscow na mmoja kati yao alirembea chupa ya mkojo juu ya baadhi ya picha hizo. Msimamizi wa tamasha hilo alisema alikuwa analifunga tamasha hilo baada ya kuapat vitisho kwa watu wadanganyifu.

Mmoja wa vijana mashuhuri wa mchezo wa  mpira wa kikapu, José Fernandez, amefariki katika ajali ya boti katika fukwe ya Miami.  Walinzi wa fukwe wa marekani wamethibitisha kuwa Fernandez ni mmoja kati ya watu watatu waliokutwa wamekufa katika majira ya mapema siku ya jumamosi baada ya doria.Klabu yake ya Miami Marlins, ilisema imeghairisha mchezo wake wa siku ya jumapili ikiwa kama ishara ya kumuenzi.  Kijana wa miaka 24 Fernandez ni mzaliwa wa Cuba.  Alijaribu kuikosoa serikali ya Cuba zaidi ya mara tatu, na akajikuta akiishia gerezani. Katika kipindi chake cha mwisho alipofanikiwa kuingia Marekani mwaka 2007, mama yake alianguka baharini Akajitosa na kufanikiwa kumuokoa.  

Mwanamme mmoja raia wa ureno ameweza kutembea kwa mara nyengine tena baada ya kutumia miaka 43 akiwa kwenye kiti cha kutembelea kutokana na utambuzi potofu wa Dawa. Mwanamme huyo Rufino Borrego, alikiambia chombo cha habari cha ureno kwamba mtaalamu wa mishipa ya hisia (neurologist) ametambua baadada ya zaidi ya miaka 40 kwamba alikuwa akisumbuliwa na maradhi tofauti kama vile myasthenia ambayo ni tofauti na utambuzi wa awali wa muscular dystrophy ambayo inatibika. Wakati Borrego alipoweza kutembea kwa mara ya kwanza kwenda kwenye mgahawa wa jirani anaokwenda kila siku uliopo Alandroal, kusinimashariki mwa ureno, mmiliki wa mgahawa huo alisema lidhani kuwa anaona muujiza mbele yake.

Beki wa Man U Chris Smalling amesema Nahodha wa timu hiyo Wayne Rooney hakuathirika kwa lolote wakati alipotupwa benchi na bado ni mchezaji bora wa Old Traford,
Rooney mwenye  umri wa miaka 30 aliachwa nje ya kikosi cha cha kwanza cha Jose Mourinho kwenye ushindi wa 4-1 dhidi ya mabingwa watetezi Leicester katika mchezo ulipigwa siku ya Jumamosi
Mlinzi huyo wa kati raia wa England ameongeza kuwa Rooney alikuwa ni yuleyule kabla ya mchezo wakati tukijiandaa na mchezo.Yeye mara nyingi amekuwa ni mjadala na alikuwa niyuleyule  tuliyemzoea.  

No comments:

Post a Comment